Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi imekamilisha uandaaji ramani za kidijitali zinatotumika kama ramani za msingi kwenye utekelezaji mfumo wa anuani za makazi katika halmashauri 38 nchini.
Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetoa siku 60 kuanzia tarehe 5 Februari 2022 kuhakikisha wamiliki wa ardhi waliopimiwa viwanja kuwasilisha maombi ya kumilikishwa ardhi huku wale wenye miliki za ardhi wawe wamelipa kodi ya pango la ardhi.
Katika kuhakikisha mlundikano wa mashauri ya migogoro ya ardhi unapungua nchini, Msajili wa Mabaraza ya Ardhi Stela Tullo ameelekeza Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya kwenda kusikiliza mashauri katika wilaya nyingine ambazo hazina wenyeviti.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ridhiwani Kikwete amelitaka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kuwa na mipango ya muda mrefu ya miradi ya ujenzi wa nyumba zake kwenye maeneo mbalimbali nchini ili kukidhi mahitaji yanayoendana na ukuaji wa miji.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ridhiwani Kikwete amewaagiza Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa mikoa nchini kuhakikisha wanawawekea vipimo vya utendaji kazi watumishi wa sekta ya ardhi kila baada ya mwezi mmoja ili kupima utendaji wao kwa lengo la kuleta tija kwenye sekta ya ardhi.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ridhiwani Kikwete amewataka wamiliki wa ardhi nchini ambao hati zao zimekamilika kujitokeza kuchukua hati zao ili waweze kupandisha tahamni ya ardhi wanayomiliki.
© 2023 All Rights Reserved.
Site Map
Staff Mail
Designed and Developed bylbl_ega_nam (e-GA) and Contents Managed by Ministry of Lands, Housing and Human Settlements Development