Jumla ya vijiji 75 vilivyokuwa na migogoro ya matumizi ya ardhi katika mkoa wa Arusha vimenufaika na hisani ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia kwake kubaki maeneo yake kufuatia vijiji hivyo kuingia kwenye migogoro ya matumizi ya ardhi na maeneo ya hifadhi.
Timu ya Wataalamu wa Mipaka kati ya Tanzania na Kenya imetembelea na kujionea kazi ya uimarishaji mipaka wa Kimataifa wa nchi hizo iliyofanywa kwa lengo la kukagua na kushauri namna bora ya kuendelea na kazi zinazofuta.
Waziri wa ardhi nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ametoa onyo kwa wananchi wanaotumia hisani ya Rais Samia Suluhu Hassan kuvamia maeneo ya hifadhi yaliyomegwa
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ridhiwani Kikwete amewataka Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya wilaya nchini kuwa waadilifu sambamba na kujiepusha na vitendo vya rushwa ili kutenda haki wakati wa kutoa maamuzi ya mashauri yanayohusu migogoro ya ardhi.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ametaka elimu na ushirikishwaji wananchi kupewa kipaumbele wakati wa utekeleza maamuzi ya Baraza la Mawiziri kuhusiana na utatuzi wa migogoro ya matumizi ya ardhi katika vijiji 975
Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa ushirikiano wake na Korea Kusini imeanzisha mkakati wa kuhakikisha inabadilisha mifumo yake upangaji, utumiaji, upimaji na uwekaji kumbukumbu za sekta ya ardhi kutoka analogia kwenda digitali ili kuboresha sekta ya ardhi.
© 2023 All Rights Reserved.
Site Map
Staff Mail
Designed and Developed bylbl_ega_nam (e-GA) and Contents Managed by Ministry of Lands, Housing and Human Settlements Development